Hii ndiyo idadi ya waliotazama kuagwa kwa Magufuli

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema kuwa karibu ya watu bilioni 4 duniani kote, wametazama kupitia vyombo vya habari zoezi la kuagwa kwa mwili wa aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli, ambalo kitaifa lilifanyika jana Jijini Dodoma.

 

Kauli hiyo ameitoa leo Machi 23, 2021, visiwani Zanzibar, wakati akivishukuru vyombo vya habari mbalimbali ambavyo vimejitoa kurusha mubashara shughuli zote za kuaga mwili wa Hayati Dkt. Magufuli.


"Nashukuru vyombo vya habari na kwa kweli mmekua nasi tangu siku ya kwanza hata tukio hili mnalirusha duniani kote, mpaka jana jioni tunazo taarifa waliofuatilia tukio la kuaga mwili wa Hayati Dkt. Magufuli, kitaifa jana Dodoma ni watu karibu bilioni 4, walikuwa wanafuatilia tukio la kuaga kwa mpendwa wetu," amesema Waziri Mkuu Majaliwa.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad