Kocha Simba Aiwekea Mtego Yanga

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




WAKATI mbio za kuwania ubingwa wa Ligi Kuu Bara zikiwa bado mbili, Kocha Mkuu wa Simba, Didier Gomes, amesema licha ya kushiriki mashindano mengi tofauti, lakini hawajasahau michezo yao mitatu ya viporo kwenye ligi hiyo ambayo wanataka kushinda ili kuishusha Yanga kileleni.

 

Hivi sasa Simba inakamata nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu Bara ikiwa imekusanya pointi 42 baada ya kucheza mechi 18, ikizidiwa pointi saba na vinara wa ligi hiyo, Yanga wenye pointi 49 zilizotokana na kucheza mechi 21 ambazo ni tatu zaidi ya Simba.



Kesho Jumatatu, Simba inatarajiwa kushuka uwanjani kuvaana na JKT Tanzania katika mchezo wa kiporo wa ligi kuu, utakaopigwa Uwanja wa Mkapa, Dar es Salaam.

 

Endapo Simba ikifanikiwa kushinda mechi zate tatu za viporo, basi itaishusha Yanga kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo na kukaa mabingwa hao watetezi kwa tofauti ya pointi mbili.

 

Akizungumza na Spoti Xtra,Gomes alisema: “Hivi karibuni ratiba yetu imetubana kidogo kwani tumekuwa na michezo mingi ya michuano tofauti, lakini ni jambo zuri kuona tunapata matokeo mazuri kwenye michezo yote.



“Licha ya michuano mingi tuliyonayo, lakini nikuhakikishie bado tunakumbuka kuwa tuna michezo mitatu ya ligi ambayo lazima tushinde, kwani tunataka kushika usukani wa ligi katika kipindi hiki ambapo ligi inaelekea ukingoni ili kujihak-ikishia malengo yetu ya kutwaa ubingwa msimu huu.”


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad