Mo Salah, kikosi cha Misri wawasili Kenya kucheza dhidi ya Harambee stars

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 



Misri na Mo Salah wamewasili jijini Nairobi Jumanne kwa ajili ya mchezo kati ya Mafarao hao na Harambee Stars, mchezo utakaopigwa katika uwanja wa michezo wa kimataifa, Kasarani Alhamisi.

Ushindi wa Misri utawahakikishia wanafuzu katika kinyang'anyiro hicho cha Afrika kitachofanyika nchini Cameroon mwaka ujao.

Kenya pia inauhitaji sana ushindi huu ili kujiongezea nafasi ya kufuzu.

Katika hatua nyingine, Mo Salah ameripotiwa na gazeti la Independent la Misri kuwa ameomba kujitenga na wenzake, lakini haijafahamika kama ombi lake limetekelezwa.

Uamuzi wa Salah wa kuishi tofauti na wenzake unaaminika kuwa jitihada za kujitenga.

Salah alikutwa na virusi vya Covi-19 wakati wa safari ya hivi karibuni barani Afrika kwa ajili ya majukumu yake ya kimichezo mwaka jana, pia mchezaji mwenzake Mohamed Elneny, anayekipiga katika klabu ya Arsenal.

Elneny pia yuko kwenye kikosi kitakachopepetana na Kenya.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad