Mwanamfalme wa Saudia na mauaji ya Kashoggi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA





Manaibu watatu kutoka Baraza la Wawakilishi la Marekani wamewasilisha mswada ambao unazingatia vikwazo kwa Mfalme wa Saudi Arabia Mohammed bin Salman (MBS) kwa madai kwamba amehusika na mauaji ya Jamal Khashoggi.
Madiwani Tom Malinowski, James McGovern na Andy Kim walitangazia Bunge la Baraza kwamba waliwasilisha muswada wenye jina "Sheria ya Dhima Kuu ya Ukiukaji wa Haki za Binadamu ya Saudi Arabia".

Katika muswada huo, ilisisitizwa kuwa katika ripoti  iliyotangazwa na Kurugenzi ya Upelelezi ya Kitaifa (DNI), ilielezwa wazi kuwa MBS alihusika na mauaji ya mwandishi wa habari wa Saudia Jamal Khashoggi na kwa hivyo anapaswa kuingizwa katika orodha ya waliowekewa vikwazo.

Muswada huo pia umesema kwamba Congress inapaswa kufahamishwa mara kwa mara juu ya ikiwa utumiaji wa silaha zilizouzwa na Marekani kwa Saudi Arabia unafuata sheria za Marekani.

Ripoti ya DNI Ijumaa ilionyesha kwamba MBS aliidhinisha mauaji ya Khashoggi, lakini utawala wa Biden haukuchukua uamuzi wowote wa vikwazo dhidi ya Mohammed bin Salman.

Wakati huo huo, Msemaji wa Ikulu Jen Psaki alisema kuwa huo ni "uamuzi sahihi" kutoweka vikwazo kwa MBS kwa mauaji ya Khashoggi na kuashiria kwamba hakuna vikwazo vitakavyowekwa hata hapo mbeleni.

"Katika historia yetu, hakuna vikwazo vyovyote vilivyowekwa kwa viongozi wa nchi ambazo tuna uhusiano wa kidiplomasia chini ya utawala wa marais wa Kidemokrasia na Republican." 

Jamal Kashogi, mwandishi wa gazeti la Washington Post na aliyejulikana kwa kumkosoa kwake Mwanamfalme wa Saudi Arabia, Mohammed Bin Salman, aliingia katika Ubalozi mdogo wa Saudi Arabia mjini Istanbul mnamo Oktoba 2 2018 na hakuonekana akitoka kamwe.

Ilibainika baadaye kwamba Kashoggi aliuawa ndani ya Ubalozi huo na kisha mwili wake kukatwakatwa vipande.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad