Ni lini Ntibazonkiza atarejea Yanga?

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Wachezaji wa klabu ya Yanga, Saido Ntibazonkiza, Tomombe Mukoko na Haruna Niyonzima wanatarajiwa kujiunga na kambi ya klabu hiyo iliyoko Avic Town Kigamboni siku ya Alhamis mara baada ya kumaliza majukumu na timu zao za Taifa.

 

Akizungumza na East Africa Radio, Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Yanga, Hassan Bumbuli amesema baadhi ya wachezaji hao wa kigeni wanamalizia mechi za mataifa yao ambayo yanawania kufuzu michuano ya mataifa ya Afrika leo na kwa mujibu wa tiketi zao wataungana na wenzao siku mbili zijazo.


''Wachezaji waliokuwa katika kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania''Taifa Stars'' walishawasili tangu siku ya Jumatatu, wakati Saido Ntibazonkiza(Burundi), Tomombe Mukoko(Dr Congo) na Haruna Niyonzima (Rwanda) wataanza kuwasili siku ya Alhamis.


Yote kwa yote timu yetu inaendela vyema na mazoezi chini ya kocha Juma Mwambusi, tupo kileleni  lakini pia bado tunaendelea na mchakato wa kumpata kocha mpya pindi ambapo tutakamilisha tutawatangazia.'' alisema Bumbuli.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad