Raila Odinga amuomboleza rafiki yake rais Magufuli

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Aliyekuwa waziri mkuu nchini Kenya na kiongozi wa upinzani Raila Odinga ametuma risala za rambirambi kwa familia ya rais John Pombe Magufuli na raia wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania.
Katika taarifa kwa vyombo vya habari Raila amemtaja marehemu kama kiongozi aliyejaribu kuimarisha hali ya raia wa Tanzania.

Amesema kwamba rais Magufuli amekuwa rafiki yake wa muda mrefu na kwamba amekuwa kando yake wakati mgumu alipomuhitaji.

Amesema kwamba tangazo la kifo chake amelipokea na huzumi kubwa akiongezea kwamba anasimama na familia ya marehemu wakati huu wa maombolezo.

Kiongozi huyo amesema kwamba kwa miaka kadhaa iliopita ameshirikiana na rais Magufuli haswa katika kuiunganisha Afrika mashariki kupitia miundo msingi.

Amewataka Watanzania wote kusalia watulivu na kufuata utamaduni uliowachwa na rais wa kwanza wa taifa hilo Julius Nyerere na wa viongozi waliofuata katika kukabidhiana mamlaka kulingana na katiba ya taifa hilo
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad