AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
ALIYEKUWA Rais wa Marekani, Donald Trump, amezungumza kwa mara ya kwanza tangu Joe Biden kuwa Rais wa nchi hiyo, na kusema kuwa hana mpango wa kuanzisha chama kipya cha siasa na badala yake ameahidi kuwa ataendelea kuungana na wana Republican.
Akizungumza akiwa Florida jana katika hotuba yake kupitia mkutano wa ‘Conservative Political Action Conference’ (CPAC), Trump amesema kitendo cha kuanzisha Chama kipya kitagawanya kura za Republican na kupelekea chama hicho kisishinde tena.
Trump ambaye aliondoka madarakani mwezi uliopita, Januari 20, 2021, amemkosoa Rais Biden kwa kubadili yaliyofanywa katika Utawala wake ikiwemo masuala ya Uhamiaji na Usalama katika mipaka.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK