Wanne wafariki kwa ajali wakitokea kwenye mapumziko

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Watu wanne akiwemo mkuu wa chuo cha uuguzi Lugarawa Steven Mtega (39) wamefariki dunia kwa kuzama kwenye mto Lupali wakiwa kwenye gari waliyokua wakisafiria kata lugarawa wilayani Ludewa mkoani Njombe.

Akizungumza kwa njia ya simu jana mganga mkuu  wa wilaya ya Ludewa dkt Stanley Mlay,alisema tukio hilo limetokea febuari 27 majira ya usiku marehemu hao walikua kwenye gari aina ya harrier ambapo walikua Lugarawa kwenye mambo yao ya mapumziko.

"Walipata ajali kwenye mto lupali huu mto sasa hivi una maji mengi kwa sababu ya mvua zinavyonyesha walikua watu wanne kwenye mambo yao ya mapumziko Lugarawa na dereva alikua huyo mkuu wa chuo wakasema wabadilishe maeneo waende Mundindi sasa walivyofika maeneo hayo ndo wanaingia mtoni" alisema Mlay.

Mlay aliwataja marehemu wengine kuwa Marko Mpete,fundi umeme wa Lugarawa
Merk Mwalongo(35)mjasiriamali
Rukia Mfaume(28) alikuwa mhasibu wa mradi wa umeme wa Akra Lugarawa

Hata hivyo alisema miili ya marehemu hao iko chumba cha kuhifadhia maiti(Mochwari)Hospital ya Lugarawa ikisubiri taratibu za mazishi kukamilishwa.

Naye diwani wa kata ya Lugarawa Erasto Mhagama,akizungumza kutokea kwa tukio hilo alisema tukio hilo limetokea mpakani kwa kijiji cha shaurimoyo na kijiji cha amani.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad