Yajue Maneno Ambayo Mke Anahitaji Kusikia Kila Siku kutoka kwako

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Mawasiliano mazuri kati ya mke na mme ni muhimu sana kwa ajili ya ustawi wa mahusiano ya wawili wapendanao. Inasemwa kuwa kuvunjika kwa mawasilioano pekee katika mahusiano kunasababisha mifarakano au kuvunjika kwa mahusaiano kati ya mke na mme kuliko sababu nyingine.

Wataalamu wa mapenzi na hisia za binadamu wanaeleza kuwa wanawake wanaguswa sana kwa maneno kuliko vitendo. Sauti na maneno mazuri ni vitu ambvyo vinawafanya wawe katika wakati mzuri sana kihisia. Wanaume wao wamefahamika kuwa wanavutwa zaidi kwa kuona kuliko kusikia.

Kwa msingi huu basi ni muhimu sana kwa wanaume walio katika mahusiano ya mapenzi kufahamu siri hii juu ya wenza wao wanawake. Ukitaka kuifanya siku ya mpenzi wako nzuri basi zingatia maneno yako na sauti yako iwe katika kiwango kinachofaa.

Yafuatayo ni maneno manne muhimu kuyasema kila siku kwa mkeo na yataleta mabadiliko makubwa katika mahusiano yenu. Maneno haya yanalainisha moyo,yanajenga uaminifu,yanazidisha upendo,yanaponya majeraha ya mapenzi na yanaleta furaha kati ya wapenzi:

1. “Wewe Ni Mwanamke Mzuri”

Inawezekana uzuri ni sababu mojawapo ya kumuoa au kuwa naye. Basi hakikisha unamkumbusha kila mara. Wanawake wanahitaji sana kuhakikishiwa kuwa ni wazuri na wanavutia. Ni hatari sana kama hufanyi hivi kwa mkeo,nakuhakikishia wanahitaji kusikia maneno haya. Usipomwambia kuna mtu atamwambia barabarani au kazini na hii ni hatari.

Wanawake wasio ambiwa mara kwa mara kuwa ni wazuri huhangaika sana juu ya kubadilisha mavazi yao na vipodozi. Ikibidi wanaweza wakafikia kuvaa mavazi yasiyo na heshima sana kwa mtazamo wa jamii anayoishi. Hii ni katika kutafuta mrejesho kuwa ni mzuri.

2. “Umependeza”

Hili linaendana na la kwanza hapo juu lakini kupendeza sio lazima uwe mzuri. Uzuri unaweza ukawa wa sura,umbo au tabia zake. Kupendeza ni kutokana na mapambo na mavazi ambayo mtu anavaa.

Kama kuna mambo makubwa ambayo yanawachukulia muda mwingi wanawake wengi basi ni urembo hasa wa mavazi,nywele na vipodozi. Wafanya biashara wajanja wanaweka nguvu zao eneo hili – kutoa huduma za wanawake.

Wanawake wanahitaji sana kuonekana wamependeza hasa toka kwa wapenzi wao.

Mrejesho huu ni muhimu kwao na kunawafanya wajisikie vizuri ,kujiamini na kujiona wa thamani. Mwambie mkeo kila siku asubuhi akitoka nyumbani au kila mnapotoka pamoja. Mwambie kila akibadilisha aina ya ususi wa nywele zake.

3: “Asante”

Kwa kweli mke ndiye mtendaji wa mambo mengi nyumbani. Hata kama kuna wasaidizi bado kunahitaji uongozi na bila shaka mke ni kiongozi wa yote haya nyumbani kwa walio wengi.

Utakuta nguo ni safi,chakula ki tayari,watoto wameoshwa na kuvalishwa na mengine mengi. Kuna kila sababu ya kusema “asante”.

Asante ina maajabu makubwa kama ikitolewa kwa jinsi inavyostahili na kwa dhati.

Kwanza humfanya anayeambiwa ajione wa thamani sana kwako. Pili humfanya anayefanya aongeze bidii kwa yale anayoyafanya.

Hivyo usiache kushukuru kila siku kwa yale mkeo anayoyafanya. Kunawezekana mengine yakawa si mazuri,lakini hakutakosekana zuri la kushukuru.

Mwambie “Asante Mpenzi” , “Asante Mke Wangu” na maisha yenu yatakuwa mazuri na yenye furaha.

Fanya kwa vitendo pia,mfano nunua hata kitenge tu na umshangaze kwa zawadi.

Mwambie “asante kwa kuwa mama mzuri wa watoto wetu” au “Asante kwa kuwa mke mzuri na rafiki mzuri kwangu”.

4: “Nakupenda”

Kupendwa ni mojawapo ya vitu ambavyo binadamu anahitaji sana. Chukulia mtoto mfano,toka tukiwa watoto kupendwa ni kitu kinachohitajika sana na kinapokosekana kuna madhara makubwa yanayotokea ikiwemo mtoto kutojipenda mwenyewe na kutojiona wa thamani. Kwa wanawake halikadharika,japo ni wakubwa tayari lakini kasumba ya utotoni imo bado ndani yetu na mahitaji ni yaleyale.

Ukiangalia vizuri mahangaiko yote ya mwanamke juu ya urembo na mavazi utaona kuwa ni kutaka kuhakikisha kuwa anapendwa. Au kujinyima na kuishi katika mwenendo ambao wewe kama mume unafikiri ni vizuri au jamii inafikiri ni vizuri ni kutaka kuhakikisha kuwa anapendwa. Basi kwa kumtamkia kuwa unampenda mara nyingi kadili utakavyoweza inampa kujiamini kwa jinsi alivyo na kwa yale anayoyafanya.

Kumwambia mkeo kuwa unampenda na kuonyesha kwa matendo kunamfanya naye akupende zaidi.

Neno hili likitumika kwa dhati na sio kusema tu lina maajabu makubwa katika kuboresha mahusiano ya wenza wapendanao.

Fanya kwa Dhati na Upendo

Maneno haya manne yana maajabu makubwa kama yakitekelezwa ipasavyo. Kwanza ni muhimu sana ukayasema kwa dhati na kumaanisha toka moyoni. Kunaweza kukawa na mambo yasiyofikia viwango vya kushukuru au kusifia lakini uanaweza ukaanza na yale machache yaliyopo. Baadae utagundua kuwa hata mengine yanarekebishwa na kufanywa kwa uzuri.

Maajabu ya maneno haya ni katika kubadilisha moyo wa mke na tabia na matendo yake. Ukiyatumia kwa kiasi kinachofaa na kwa kuyamaanisha utafanikiwa na utaboresha mahusianao yenu.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad