Bobi Wine atakiwa kulipa kiasi hiki cha fedha ili arudishiwe gali lake la kifahari linaloshikiliwa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Mamlaka ya mapato nchini Uganda (URA), imemtaka kiongozi wa upinzani na mgombea wa uchaguzi Robert Kyagulanyi, al maarufu Bobi Wine, kulipa ushuru ya shilling za Uganda milioni 337 sawa na dola 166,700, ili arudishiwe gari lake la land Cruiser.



Taarifa ya uamuzi huo kwa kiongozi wachama cha National Unity Platform (NUP) inakamilisha mchakato wa mamlaka ya forodha nchini humowa kutathmini thamani ya gari hilo linalozuia risasi, ambalo awali lililipiwa ushuru mdogo kwa kulinganishwa na gari lingine la kawaida.

Akijibu juu ya hatua kuthamanishwa upya kwa gari lake kupitia ujumbe wake wa twitter, Bobi Wine amelalamikia hatua hiyo.

‘’Baada ya majaribio kadhaadhidi ya maisha yangu, baadhi ya marafiki zangu walinipatia gali linalozuia risasi. Mara ya kwanza mambo yote alikuwa mazuri kwasababu halikwa kwa jina langu. Interpol, Idara ya uchunguzi ya polisi na URA wote walilichunguza na kuliidhinisha . Ushuru unayotozwa na URA tuliilipa. Mambo yalianza kugeuka wakati walipogundua kuwa ni gari langu’’ amesema:


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad