Fahamu kuhusu ugonjwa wa Polio kiundani zaidi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Polio ni ugonjwa wa kuambukiza usababishwao na virusi, huathiri neva na kusababisha ulemavu. 

Kutokana na taarifa za shirika la afya duniani: 
Polio huathiri zaidi watoto wa umri wa chini ya miaka mitano 
Ulemavu hutokea kwa mmoja kati ya maambukizi 200 
Mpaka 2013 ni nchi tatu ambazo bado kuna mlipuko wa ugonjwa huu wa kupooza Afghanistan, Pakistan na Nigeria. Ila kutokana na Taarifa kutoka wizara ya afya ya Tanzania ilipokea taarifa kutoka shirika la afya duniani kuwa kuna mlipuko katika nji jirani ya Kenya, wilaya ya Fafi. 

Je ni zipi dalili za ugonjwa huu? 
Dalili hizi hudumu kwa kati ya siku 1 hadi 10 
Homa 
Maumivu ya kichwa 
Kutapika 
Uchovu 
Maumivu ya shingo 
Maumivu ya mgongo 
Maumivu ya mikono na miguu 
Misuli kukakamaa 

Je ni matatizo gani mtu huweza kupata baada ya maambukizi haya? 
Kupooza misuli 
Ulemavu wa miguu 

Vipimo: 
Virusi vya polio huweza kuonekana katika makohozi, kinyesi na maji maji ya uti wa mgongo. 

Matibabu 
Hamna matibabu ya maambukizi haya, kwahiyo ni tiba ya dalili ambayo hutolewa: 
Kupumzika 
Dawa za kutuliza maumivu na kushusha homa 
Antibiotiki kuzuia maambukizi nyemelezi 
Mazoezi kiasi kwaajili ya kuzuia kukakamaa 
Na kula chakula bora 

Kinga 
Ni chanjo ya Polio ambayo hutolewa pamoja na chanjo nyingine kwa watoto baada tu ya kuzaliwa, na kurudiwa tena katika wiki ya nne, ya nane na mwisho ya kumi na mbili. 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad