Kauli ya rais wa Marekani Biden, hatimaye haki imetendeka, Ubaguzi ni doa kwa roho ya taifa lote

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 
“Tutaongeza juhudi kuhakikisha mengine yanafikiwa. Hii itakuwa hatua ya kwanza muhimu ya kukabiliana na ubaguzi wa rangi uliokithiri katika mifumo yetu,” rais alisema.



Na katika hotuba ya kitaifa iliyopeperushwa kwenye runinga muda mfupi baadaye, Bwana Biden alisema: “Ubaguzi wa kimfumo ni doa kwa roho ya taifa lote.”

Rais wa Marekani Joe Biden
Wakati huo huo, Bi Harris aliwahimiza wabunge kupitisha muswada wa George Floyd unaolenga kurekebisha idara ya polisi nchini Marekani . “Muswada huu ni sehemu ya urithi wa George Floyd. Kazi hii ni ya muda mrefu,” alisema.

Shirikisho la polisi la Minneapolis, shirika lisilo la faida linalowakilisha polisi – lilishukuru jopo la waliotoa uamuzi huo kwa “kazi yao ya kujitolea” kubeba “mzigo mkubwa”.

Shangwe katika viwanja vya Black Lives Matter Square, Washington
“Tunataka pia kufikia jamii na bado tueleze masikitiko yetu makubwa kwa maumivu yao, kwani tunayahisi kila siku pia. Hakuna washindi katika kesi hii na tunaheshimu uamuzi wa majaji,” shirikisho lilisema.

“Tunahitaji kutuliza siasa na kukomesha harakati za viongozi waliochaguliwa kukoma kuendelea kuzua uhasama kwa msingi wa rangi.”

Chauvin anatarajiwa kukata rufaa dhidi ya uamuzi huo, kulingana na ripoti za vyombo vya habari nchini Marekani.

Wanasema njia moja ya uwezekano wa kukata rufaa ni utangazaji mkubwa uliotolewa kwa kesi hiyo, na timu ya utetezi ikisema kwamba hii inaweza kuwa imeathiri majaji.

Pia, Jaji aliyeongoza kesi hiyo Peter Cahill alisema Jumatatu kwamba maoni yaliyotolewa na Mwanasiasa wa Democrat Maxine Waters yanaweza kuwa sababu ya kukata rufaa.

Mwishoni mwa wiki, Bi Waters alikuwa amewataka waandamanaji “kusalia barabarani” na “kuzua malalamiko zaidi” ikiwa Chauvin ataachiliwa.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad