Kirusi Kipya cha Covid 19 ni Hatari Zaidi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




SHIRIKA  la Afya duniania WHO limesema aina ya virusi vya corona ambavyo vinahofiwa kuchangia wimbi la visa vya maambukizi nchini India vimebainika katika mataifa mengine kadhaa duniani.

 

Shirika hilo la Umoja wa Mataifa limesema kirusi aina ya B.1.617 vya Covid-19 ambavyo kwa mara ya kwanza viligundulika India, kwa rekodi za jana vilibainika katika mataifa mengine takribani 17.

 

Taarifa hiyo ilisema idadi kubwa ya visa vyake vya maambukizi vimetokea Uingereza, Marekani na Singapore.

 

Kwa namna inavyotambulishwa aina hiyo ya virusi inaonesha kuwa ni hatari zaidi kuliko ile ya awali ikioneshwa kuwa na uwezo wa kuwa na kasi ya maambukizo au kuweza kukwepa kinga za chanjo.

 

Mlipuko wa maambukizi wa India kwa rekodi za jana pekee umesababisha visa vipya 350,000, hali inayosababisha rekodi mpya ya maambukizo duniani kufikia watu milioni 147.7 na vifo zaidi ya milioni 3.1.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad