Kisa cha LaMarcus kustaafu NBA kinasikitisha

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Nyota wa Brooklyn Nets, LaMarcus Aldridge ametangaza kustaafu kucheza mchezo wa mpira wa kikapu ligi kuu nchini Marekani NBA kutokana na maradhi ya moyo yanayomsumbua akiwa mchezoni.

 

LaMarcus ametangaza hivyo usiku wa kuamkia leo kupitia akaunti zake za kijamii akiandika “Huu ni muda wa kuweka afya na familia yangu mbele, Japo naendelea vizuri kwasasa lakini nilijisikia vibaya zaidi usiku ule kitu ambacho ni tishio zaidikuwahi kutokea kwenye maisha yangu”.


LaMarcus ambaye aliwahi kukipiga kwenye vilabu vya Portland Trail Blazers na San Antonio Spurs amestaafu akiwa na umri wa miaka 35 tena akiwa na wastani wa alama 19.4 na rebaundi 8.2 ambacho kimemsaidia kuzidi kujizolea mashabiki wengi tokea ajiunge na Nets mwezi uliopita.


 (Mkurugenzi wa NBA, Adam Silver.)


Miongoni mwa watu waliotoa salam za pole na kutambua uwezo wa nyota huyo ni, Mkurugenzi wa NBA, Adam Silver ambaye amesema, “Afya yake ya leo  na baadaye ni muhimu zaidi kuliko mchezo wenyewe, na tunajua haukuwa uamuzi mrahisi kwake”.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad