Mtaalamu wa mapafu asema Floyd alikufa kwa kukosa hewa ya Oksijeni

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA





Upande wa mashtaka katika kesi kuhusu kifo cha Mmarekani mweusi George Floyd aliyekufa kwa kugandamiziwa goti shingoni na polisi Mzungu, umesema uchunguzi wa kitaalamu umeonesha kuwa Floyd alikufa kutokana na kukosa hewa ya oksijeni. 
Shahidi wa upande huo ambaye ni daktari wa mapafu, Martin Tobin, amesema kukosa hewa hiyo ndiko kulikoufanya moyo wa marehemu kusimama, na amekosoa madai ya upande wa utetezi wa polisi anayeshutumiwa kumuuwa Floyd, Derek Chauvin, kwamba magonjwa aliyokuwa nayo George Floyd yalichangia katika kifo chake. 

Mkanda wa vidio uliosambaa duniani, ulimuonesha Chauvin akigandamiza goti lake katika shingo ya Floyd kwa muda wa takribani dakika tisa.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad