Polisi auawa kwenye shambulizi karibu na majengo ya bunge

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA





Mtu mmoja amepigwa risasi na kufariki baada ya kuvurumisha gari kwa maafisa wawili wa polisi karibu na majengo ya bunge nchini Marekani Capitol. Afisa mmoja wa polisi amekufa kufuatia kisa hicho.

Mshukiwa wa shambulizi hilo, alivurumisha gari dhidi ya maafisa wawili wa polisi waliokuwa wakishika doria katika majengo ya bunge ya Marekani yaliyoko Capitol mjini Washington DC, kabla ya kupigwa risasi na maafisa.

Shambulizi hilo limefanyika karibu na mahali ambapo wafuasi wa Donald Trump waliingilia majengo ya bunge na kuyavamia mnamo January 6 mwaka huu.

Kilichofanyika

Maafisa wa polisi wamesema gari hilo lililovurumishwa dhidi ya maafisa wa polisi liligonga vizuizi vya usalama, kisha mshukiwa aliyekuwa akiliendesha akatoka nje akiwa amebeba kisu mkononi na kukimbia kuelekea kwa maafisa wa polisi.

Mshukiwa huyo alikaidi amri kutoka kwa maafisa wa usalama na ndipo wakampiga risasi. Alifariki baadaye hospitalini.

Maafisa wawili waliohusika pia walikimbizwa hospitalini ambapo mmoja alifariki.

”Ni kwa masikitiko makubwa tunatangaza kuwa afisa wetu mmoja amefariki kutokana na majeraha,” amesema Yogananda Pittman, kaimu mkuu wa polisi wa Capitol.

”Tafadhali mkumbukeni kwenye maombi yenu,” amesema Pittman kwenye taarifa.

Kisa hicho kimetokea takriban mita 90 kutoka katika lango la Kaskazini la kuingia majengo ya bunge upande wa baraza la seneti, ambalo hutumika na maseneta pamoja na maafisa siku za kazi. Kwa sasa bunge liko likizoni.

Rais Biden asikitishwa na shambulizi pamoja na kifo cha afisa

Rais wa Marekani Joe Biden ambaye hayuko mjini Washington kwa sasa amesema  yeye pamoja na mke wake Jill Biden wamesikitishwa na shambulizi hilo.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad