Urusi yaijibu Marekani kwa kuwatimua wanadiplomasia wake

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA





Urusi imewataka wanadiplomasia 10 wa Marekani kuondoka nchini humo katika hatua ya kulipiza kisasi baada ya Marekani kuwafukuza wanadiplomasia 10 wa Urusi kwa madai ya udukuzi na kuingilia kati uchaguzi wa Marekani wa mwaka uliopita.

Wizara ya mambo ya nje ya Urusi imesema John Sullivan, ambaye ni balozi wa Marekani nchini Urusi, anapaswa kurudi nyumbani katika kile walichosema ni kwa mashauriano zaidi.

Kupitia taarifa, wizara ya mambo ya nje ya Urusi imesema huu ni wakati wa Marekani kuonyesha ukomavu wake wa kiakili na kugeuza mkondo wao wa kugombana.

Taarifa hiyo imeongeza kusema kuwa ina uwezo wa kuiumiza zaidi Marekani kuichumi na kupunguza idadi ya wanadiplomasia wa Marekani nchini Urusi hadi 300, japo kwa sasa haitachukua hatua hiyo.

Uamuzi wa Urusi, ukiwa sehemu ya mpango mpana wa kulipiza kisasi, uliidhinishwa na Rais Vladimir Putin kama jibu kwa Marekani baada ya serikali ya Joe Biden kuiwekea vikwazo Urusi.

Hata hivyo licha ya Moscow kujibu kwa haraka na kuweka hatua ambazo zinanuia kupunguza ushawishi wa Marekani nchini Urusi, Urusi imeacha mwanya wa mazungumzo uliopendekezwa na Rais Joe Biden aliyetaka kufanyika mkutano kati yake na Putin ili kujadili masuala kadhaa.

Credit:BBC 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad