Wawa: Hakuna wa Kuzuia Ubingwa Simba

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA






BEKI wa kati wa Simba, Muivory Coast, Pascal Wawa ameibuka na kuweka wazi kuwa kutokana na ubora wao kwa sasa haoni atakayeweza kuwazuia kutetea ubingwa wao msimu huu katika Ligi Kuu Bara.

 

Wawa ametoa kauli hiyo kufuatia Simba kufanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 5-0 dhidi ya Mtibwa Sugar katika mchezo wa ligi kuu uliopigwa juzi Jumatano kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar.

 

Akizungumza na Championi Ijumaa, Wawa alisema: “Nadhani bado tupo kwenye ubora ndiyo jambo kubwa la kumshukuru Mungu kwa sababu licha ya ushindani na ugumu wa ligi lakini bado tumekuwa na uwezo wa kupata matokeo bora zaidi kwa upande wetu.

 

“Kiukweli naamini nafasi ya kutetea ubingwa wetu ipo wazi na hakuna ambaye anaweza kuzuia hilo kwa sasa kutokana na kuwa kwenye kiwango bora cha ushindani, kitu kikubwa ambacho tunakifanya kwa sasa ni kushinda mechi zetu ili malengo yatimie bila ya kuangalia nani anaongoza ligi,” alisema Wawa.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad