Bondia Ashtakiwa kwa Kumuua Mpenzi wake mjamzito

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Bondia wa Puerto Rico aliyepigana katika michezo ya Olimpiki ya London mwaka 2012 ameshtakiwa kwa kumteka na kumuua mpenzi wake aliyekuwa mjamzito.

Félix Verdejo anatuhumiwa kwa kumshambulia na kumuua Keishla Rodríguez kisha kuutupa mwili wake chini ya daraja karibu na San Juan,mji mkuu wa eneo hilo la kisiwani lilipo chini ya himaya ya Marekani.

Alijisalimisha kwa polisi siku ya Jumapili baada ya kukataa kushirikiana na wachunguzi, polisi imesema.

Kifo hicho kiibua maandamano kupinga mauji dhidi ya wanawake huko Puerto Rico.

Mwezi Januari, kisiwa hicho kilitangaza hali ya hatari kufuatia dhulma dhidi ya wanawake. Puerto Rico huripoti angala kisa kimoja cha mauji ya mwanamke kila wiki, kwa mujibu wa kundi la kutetea haki nchini, huku visa vingine 60 vy auhalifu wa aina hiyo vikiripotiwa mwaka jana.

Bondia huyo mwenye umri wa miaka 27- anakabiliwa na mashtaka ya utekaji, wizi wa gari ulisababisha kifo na kuua kwa kukusudia mtoto ambaye hajazaliwa.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad