Maelfu ya watu wakimbia Goma kuhofia mlipuko mpya wa volkano

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Mamlaka nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) zimeamuru wakaazi wa mji wa Goma ulio na watu milioni mbili kuondoka katika maeneo yao kwa hofu ya mlipuko wa pili wa volcano.

Siku ya Jumamosi, Mlima Nyiragongo ulilipuka na kusababisha maafa kwa maisha na mali za watu.

Amri ya watu kuondoka inakuja baada ya onyo kutolewa kuhusu uwezekano wa kutokea kwa milipuko mingine ya volcano katika mlima huo na chini ya Ziwa Kivu lililo karibu.

Tayari makumi ya maelfu ya wakaazi wa mji huo wameshayakimbia makaazi yao ili kunusuru maisha.

Kwa mujibu wa mamlaka ni wakazi wa wilaya 10 ambao wanahamishwa.

"Hii inaweza kutokea hata bila onyo lolote" na inaweza kuwaweka wakazi katika hatari inayohusishw ana mtiririko wa lava, alisema Jenerali Costant Ndima, Gavana wa kijeshi wa eneo la Kivu- Kaskazini .


"Shughuli ya uokoaji lazima ifanyike kwa umakini chini ya uratibu wa wafanyakazi wa kibinadamu.

"Watu watarejea nyumbani baada ya mapendekezo ya mamlaka ya," aliongeza.

Gavana wa jimbo hilo pia ametoa wito kwa wakazikukaa mbali na mtiririko wa lava.

Tunapendekeza watu wakae mbali na lava ambayo ni hatari na inaweza kuua mtu kukosa hewa au kuchoma.

Hatari zingine ni mchanganyiko wa maji na lava ni aina tofauti: mchanganyiko wa uji uji wa na maji ya ziwa, unapunguza kiwango cha gesi kinachoyeyushwa chini ya maji ya Ziwa Kivu, hali ambayo huenda ikasababisha kuenea kwa gesi hatari kwa watu walio karibu.

Wakazi wameshauriwa kuzingatia maelekezo wanayopewa na kuwa waangalifu

Pia wameombwa "kubeba vitu kidogo ili kila mmoja apate nafasi" katika magari ambayo yatatolewa na mamlaka ya mkoa katika kila wilaya.

Mlima Nyiragongo mara ya mwisho ulilipuka mwka 2002, kuua watu 250 na kuwaacha wengine 120,000 bila makao. Mlipuko hatari zaidi wa volkano ulifatokea mwaka 1977, ambapo zaidi ya watu 600 people walifariki.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad