Mshukiwa wa utapeli wa mamilioni ya pesa akiwa Marekani kufikishwa mahakamani Kenya

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA





Stacey Marie Parker anatuhumia kuwatapelli Wakenya mamilioni ya fedha huku akidai watapata faida zaidiImage caption: Stacey Marie Parker anatuhumia kuwatapelli Wakenya mamilioni ya fedha huku akidai watapata faida zaidi
Mwanamke anayeshukiwa kuwa ndiye msimamizi wa mpango wa utapeli ambao ulitumiwa kuwalaghai Wakenya mamia ya mamilioni ya pesa amekamatwa mwishoni mwa wiki na atafikishwa mahakamani leo.

Stacey Marie Parker mwenye umri wa miaka 50, alikamatwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta Jumamosi alipowasili kutoka Marekani.

Mshukiwa alikamatwa kufuatia uchunguzi ulioendeshwa na idraa ya makosa ya Jinai nchini Kenya baada ya kuhusishwa na sakata hiyo ya ulaghai iliyopora pesa wawekezaji ambao hawakujua kwamba wanahadaiwa.

Katika mpango ulioratibiwa na kupangwa vizuri, wawekezaji walidanganywa kuwekeza pesa zao katika programu ya mtandaoni inayojulikana kama Amazon Web Worker, kwa kudhani kuwa watapata faida kubwa ya hadi 38% kwa amana inayodumu kwa siku 7 tu.

Kumbi za mitandao ya kijamii zilikuwa zimejaa matangazo yaliyowashawishi Wakenya kujiunga na mpango huo ili wapate faida .

Wakenya wasio ambao hawakujua kwamba mpango huo ulikuwa utapeli walipakua programu kwa wingi na wakasajiliwa huku wengi wakiweka amana zao. Wengine waliwapeleka wapendwa wao , watoto na marafiki wa karibu kwenye mpango huo, kwa nia ya kupata utajiri wa haraka.

Hadi wakati programu hiyo ilipofutwa kutoka mtandaoni bila taarifa kwa wawekezaji , ndipo wawekezaji walipogundua walikuwa wamedanganywa.

Walishtuka kujua kwamba programu hiyo haikuhusishwa kwa njia yoyote na Amazon, kampuni ya teknolojia ya kimataifa iliyo nchini Marekani Programu hiyo ilizama na amana zenye thamani ya mamia ya mamilioni ya pesa .
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad