Papa Francis atuma ujumbe Cologne kuchunguza unyanyasaji wa kingono

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA





Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis amewatuma wajumbe wawili kwenda katika Kanisa la Cologne, Ujerumani kuchunguza iwapo jimbo hilo lilifanya makosa katika kushughulikia kashfa za udhalilishaji wa kingono. 
Mwakilishi wa Vatican nchini Ujerumani, Nikola Eterovis amesema Papa Francis ameamuru wajumbe hao Askofu wa Stockholm, Kadinali Anders Arborelius na Askofu wa Rotterdam, Johannes van der Hende kuchunguza makosa yanayowezekana kufanywa na Askofu Mkuu wa Cologne, Rainer Maria Woelki.

 Maaskofu hao wataizuru Cologne mwezi ujao na watafanya uchunguzi wao kwa muda wa wiki mbili. Uchunguzi wa kashfa hiyo uligundua zaidi ya visa 300 vya udhalilishaji wa kingono katika kanisa dhidi ya watoto waliokuwa chini ya miaka 14 kati ya mwaka 1975 na 2018. 

Zaidi ya wanyanyasji 200 walihusika kuwadhuru watoto. Ripoti ya mwezi Machi iligundua kuwa maafisa wa kanisa walikiuka majukumu yao katika kukabiliana na visa hivyo.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad