Britney Spears Alilia Uhuru wake Akidai Kunyimwa haki na babake Kupata Watoto zaidi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Nyota maarufu wa muziki nchini Marekani Britney Spears amezindua shambulio kali juu ya agizo la usimamizi wa mali na maisha akisema ni "dhuluma" ambazo zimedhibiti maisha yake kwa miaka 13.


Alisema alikuwa ameumia na kulia kila siku, akimwambia jaji huko Los Angeles: "Nataka maisha yangu yarudi tu".

Spears, 39, pia alisema alikuwa amenyimwa haki ya kupata watoto zaidi na aliwekwa kwenye dawa ya lithiamu ya akili kinyume na matakwa yake

Baba yake alipewa udhibiti wa mambo yake kwa amri ya korti mnamo 2008.

Amri hiyo ilitolewa baada ya nyota huyo kuwekwa hospitalini wakati wa wasiwasi juu ya afya yake ya akili, na imeongezwa kwa zaidi ya muongo mmoja tangu wakati huo .

Kikao cha Jumatano ndio mara ya kwanza Spears kusema katika korti wazi juu ya kesi yake. Jaji wa Mahakama Kuu ya Los Angeles Brenda Penny alishukuru Spears kwa maneno yake "ya ujasiri" wakati wa kesi hiyo.

Ilifuatia uvumi mwingi juu ya hali ya nyota huyo wa muziki wa pop, na mashabiki wakitafuta kwa hamu matokeo ya kesi hiyo katika kumbi zake za mitandao ya kijamii. Harakati inayoongozwa na mashabiki, inayojulikana kama #FreeBritney, imefanya kampeni ya uhuru wake wa kisheria kwa miaka.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad