Chanzo Cha Kifo Cha TB Joshua Aliyefariki Baada ya Kutoka Kuhubiri

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA





Mhubiri wa kimataifa, Temitope Balogun Joshua maarufu TB Joshua amefariki dunia jana Jumamosi Juni 5, 2021 nchini Nigeria.

Taarifa iliyotolewa na kanisa lake la Scoan inaeleza kwamba TB Joshua alifariki muda mfupi baada ya kutoa huduma katika kanisa hilo Jumamosi.

TB Joshua alizaliwa mwaka 1963 na mpaka anakutwa na mauti alikuwa na umri wa miaka 58.

"Jumamosi Nabii TB Joshua alizungumza katika mkutano wa washirika kupitia Emmanuel TV alisema 'kila jambo na wakati wake, kuna wakati wa kuja hapa kwa maombi na wakati wa kurudi nyumbani baada ya ibada'."

"Mungu amemuita nyumbani Nabii TB Joshua kwa mapenzi yake. Nyakati zake za mwisho hapa duniani alizitumia katika huduma ya Mungu. Hiki ndio kitu alichozaliwa kukifanya, alikiishi na kukifia," inaeleza taarifa hiyo.

Hata hivyo, taarifa hiyo haijaeleza chanzo cha kifo chake huku ikiwataka waumini kumwombea mhubiri huyo na kuwapa nafasi wanafamilia kuomboleza kifo cha mpendwa wao.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad