Meli Kubwa ya Jeshi la Wanamaji la Iran yateketea na Kuzama Baharini

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA





Meli kubwa kabisa ya jeshi la wanamaji la Iran imeteketea na baadae kuzama hii leo katika mazingira yasiyoeleweka kwenye ghuba ya Oman.
Hayo yameripotiwa na mashirika ya habari ambayo hayamilikiwi moja kwa moja na serikali. Mashirika hayo ya Fars na Tasnim yameeleza kwamba juhudi za kuiokoa meli ya Kharg zimeshindwa.

Kwa mujibu wa taarifa za kituo cha televisheni ya taifa wazima moto walijaribu kuudhibiti moto huo. Meli hiyo iliyopewa jina la kisiwa ambacho ndio kituo kikubwa cha mafuta cha Iran,Kharg, ilizama karibu na bandari ya Jask kiasi kilomita 1,270 Kusini mashariki mwa Tehran katika ghuba ya Oman karibu na mlango bahari wa Hormuz.

Picha zinazosambaa katika mitandao ya kijamii nchini Iran zinaonesha mabaharia wakiwa wamevaa jaketi za kujiokoa wakiondoka kwenye meli hiyo huku moto ukiwaka.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad