Usajili wa Manyama Azam kama Wijnaldum na PSG

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Klabu ya soka ya Azam imemtambulisha rasmi mlinzi Edward Manyama kuwa mchezaji wao mpya kwa mkataba wa miaka 3 akitokea Ruvu Shooting.


Manyama ambaye ni mchezaji wa timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ alikuwa anahusishwa kujiunga mabingwa wa soka nchini Tanzania Simba, ili akasaidiane na Mohamed Hussein Tshabalala


Lakini katika hali ya mshangao beki huyo ametambulishwa upande wa Azam ili akasaidiane na Mzimbabwe Bruce Kangwa ambaye kwa sasa uwezo wake unaonekana kupungua siku hadi siku.


Si mara ya kwanza kwa Manyama kuwashangaza watu katika usajili wake, wakati wa dirisha dogo aliondoka ghafla ndani ya kikosi cha Namungo pamoja na kutoa mchango mkubwa kwa timu hiyo kufuzu hatua ya makundi ya kombe la shirikisho akaenda kujiunga Ruvu Shooting.


Suala la Manyama linafanana kwa kiwango fulani na usajili wa kiungo wa zamani wa Liverpool Georginio Wijnaldum kukaribia kujiunga na Barcelona,lakini ghafla akatangazwa upande wa PSG.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad