Dereva amuua kondakta wakigombania abiria

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA





Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma linamshikilia Dereva wa Daladala (jina linahifadhiwa) kwa kosa la mauaji ya Kondakta wa daladala, Juma Hamisi (25) wakati wakigombea abiria.

Akizungumza na Waandishi wa Habari, leo Alhamisi Julai Mosi, 2021 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Onesmo Lyanga amesema Mtuhumiwa alitenda kosa hilo Juni 15, 2021 katika Mtaa wa Mji Mpya jijini Dodoma ambapo alimuua kwa kumpiga na jiwe kichwani wakati wakigombea abiria katika eneo hilo.

Kamanda Lyanga amesema dereva huyo mara baada ya kumuona abiria walianza kumgombea na marehemu kila mmoja akitaka aingie katika gari yake.

Amesema mara baada ya msako Juni 19, mwaka huu wamefanikiwa kumkamata dereva huyo akiwa mafichoni katika Kijiji cha Galapo Wilaya ya Babati, Mkoa wa Manyara.


 
Kamanda Lyanga amesema mtuhumiwa anatarajia kufikishwa mahakamani kwa kosa la mauaji.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad