Wahamiaji 368 wa Kiafrika waokolewa na walinzi wa pwani ya Morocco

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Wahamiaji 368 wasio wa kawaida, wengi wao wakiwa raia wa Kiafrika, waliokolewa katika pwani ya Morocco.

Kulingana na taarifa ya shirika rasmi la habari la Morocco MAP, iliyotolewa na afisa mmoja, vitengo vya walinzi wa pwani viliwaokoa wahamiaji 368 wasiokuwa wa kawaida mnamo 20-23 Julai.

Wahamiaji wasio wa kawaida waliokuwa wakijaribu kwenda Ulaya kutoka Afrika, walijipata hatarini kwa kutumia boti 22 za hewa, boti 30 za kawaida na mipira 5 ya baharini ambayo walitumia.

Wahamiaji wasio wa kawaida waliookolewa kutoka pwani ya Morocco walifikishwa kwa mamlaka husika kwa utekelezaji wa taratibu muhimu baada ya huduma ya kwanza.

Kila mwaka, maelfu ya wahamiaji wasio wa kawaida husafiri kutoka Afrika kwenda Mediterania kufikia Ulaya kwa matumaini ya maisha bora, wengine wao wanafanikiwa kufika Ulaya, wakati wengine hufa baharini.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad