google-site-verification: googleb0bc30c3e5fdb812.html Aliyetaka Kujilipua Kwenye Mazishi Akamatwa | UDAKU SPECIAL

Aliyetaka Kujilipua Kwenye Mazishi Akamatwa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA







MSHAMBULIAJI anayeshukiwa kuwa wa kujitoa muhanga amekamatwa nchini Uganda kwa kupanga kujilipua katika mazishi ya kamanda wa jeshi anayefahamika kama ‘they lion of Mogadishu’’.

 

Meja Jenerali Paul Lockech alipewa jina hilo la bandia tangu wakati alipokuwa Mkuu wa kikosi cha Muugano wa Afrika kilichopo nchini Somalia (Amisom) kuanzia mwaka 2000. Alisifika kwa kuwaondosha wanamgambo wa al-Shabab katika mji mkuu Mogadishu.

 

Amisom kilisema kuwa itamkumbuka kama “ mnara wa ishara ya heshima katika mapigano dhidi ya wanamgambo wenye silaha” , na kwamba atakumbukwa kama urithi ambao hauwezi kusahaulika.

 

Meja Jenerali Lokech mwenye umri wa miaka 55, ambaye alikuwa anafanya kazi akiwa Inspekta Jenerali wa polisi alifariki kutokana na ugonjwa wa kuganda kwa damu nyumbani kwake siku ya Jumamosi.

 

Rais Yoweri Museveni amekuwa akitarajiwa kuhudhiria mazishi yake katika wilaya ya kaskani Mwa nchi hiyo ya Pader. Mshukiwa alikamatwa Alhamisi mchana katika operesheni ya pamoja baina ya maafisa mbalimbali wa usalama.

 

Msemaji wa jeshi Flavia Byekwaso amesema kuwa alipatikana na zana za kutengeneza mabomu, ikiwa ni pamoja na mabegi ya mabomu, fulana za mabomu ya kujitoa muhanga, na kifaa cha kukata waya wa kulipua mabomu. Washukiwa wenzake pia wametambuliwa na operesheni bado inaendelea ili kuwapata, alisema.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad