Kipchoge shujaa aliyeacha alama Olimpiki

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Eliud Kipchoge amesema ametimiza azma yake ya kuacha alama, baada ya mwanariadha huyo wa Kenya kufanikiwa kuwa mwanaridha wa kwanza tangu mwaka 1980 kutetea medali ya dhahabu  katika Olimpiki, baada ya kushinda mbio za marathoni za Tokyo 2020.

Kipchoge, ambaye anachukuliwa kama mwanariadha bora wa wakati wote, anakuwa mwanariadha wa tatu kushinda mara mbili mbio za marathoni katika Olimpiki, na alimaliza mbio hizo za Tokyo 2020 kwa kutumia muda wa saa mbili dakika nane na sekunde 38.

“Nadhani kwa kushinda marathoni mara mbili mfululizo nimefanikiwa kuweka alama na urithi, sasa nategemea itasaidia kuhamasisha kizazi kijacho,” alisema Kipchoge akiongea na vyombo vya habari vya kimataifa.

Kufuatia ushindi wa mwanaridha huyo maarufu, mitandao ya kijamii nchini Kenya imejaa pongezi kwa Kipchoge huku wakipendekeza kwa Rais Uhuru Kenyatta kumjengea sanamu mwanariadha huyo kutokana na heshima aliyoiletea nchi hiyo na Afrika kwa jumla.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad