"Mbowe alifunguliwa kesi mwaka jana" Rais Samia

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA anayekabiliwa na kesi za uhujumu uchumi na ugaidi, kesi yake hiyo ilikuwa imefunguliwa  tangu Septemba mwaka 2020 lakini uchunguzi ulikuwa bado unafanyika dhidi yake.

Rais Samia ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na BBC Swahili, ambapo ameongeza kuwa kwa kipindi chote hicho upelelezi wa kesi zake ulikuwa bado haujakamilika lakini wapo wenzake katika kesi hiyo uchunguzi ulikwishakamilika na wanatumikia hukumu zao.

"Mbowe kipindi kirefu hakuwepo nchini, alikuwa Nairobi, lakini alivyoingia tu nchini akaitisha maandamano na madai ya Katiba, nadhani ni calculations akijua kwamba ana kesi ya aina hiyo na hii vurugu anayoifanya akikamatwa aseme mmh! kwa sababu ya Katiba, lakini kwa vile jambo lipo mahakamani sina uhuru wa kulizungumzia nadhani tuiachie Mahakama zioneshe ulimwengu kwamba hizo shutuma ni za kweli ama si za kweli," amesema Rais Samia.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad