Miquisone Afanyiwa Kufuru Misri

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA





HABARI ikufikie kwamba, Klabu ya Al Ahly ya Misri, itakuwa inamlipa Luis Miquissone mshahara wa kufuru ambao unatajwa kuwa ni takribani mara nane aliokuwa akipewa ndani ya Simba.


Miquisone ambaye alijiunga na Simba, Januari 2020, tayari ameuzwa na timu hiyo kwenda Al Ahly.Akiwa Simba, kiungo huyo raia wa Msumbiji, alikuwa akipokea zaidi ya shilingi milioni nane kwa mwezi, lakini huko Al Ahly atapokea zaidi ya shilingi milioni 60.

 

Chanzo kutoka ndani ya Simba, kimelieleza Spoti Xtra kwamba, pamoja na Simba kunufaika na pesa ya uhamisho wa kiungo huyo, jambo lililomvutia Miquisone kwenda Al Ahly ni mshahara aliotangaziwa na Waarabu hao.

 

“Ujue watu wengi hawajui kisa cha mabosi wetu Simba kuamua kumuuza Miquissone, huyu mchezaji kaiingizia klabu yetu takribani shilingi bilioni mbili.“

 

Uhamisho wake ulitokana na ushawishi alioupata baada ya kuwekewa mshahara mnono ambao ni zaidi ya mara nane aliokuwa akipewa na Simba, hivyo akajikuta anaomba uongozi umruhusu kuondoka.“Hivyo kama viongozi hawakuwa na budi kumruhusu maana hata kama wangemkatalia kulikuwa na uwezekano mkubwa baadaye kuondoka bure au kwa dau dogo,” kilisema chanzo chetu.

Stori: MUSA MATEJA, Dar es Salaam
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad