Mwanamke mmoja afariki 'baada ya kupata chanjo ya Pfizer' New Zealand

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA





New Zealand imeripoti kile inachoamini kuwa kifo cha kwanza kinachohusisha chanjo ya corona ya Pfizer.
Bodi huru inayoangazia usalama wa chanjo nchini humo imesema kifo cha mwanamke huyo ''pengine'' ni kutokana na maumivu ya misuli ya moyo.

Pia imesema kulikuwa na changamoto nyingine ambazo kuna uwezekano zilisukuma athari za chanjo kutokea.

Waangalizi wa Ulaya wamesema kuwa ugonjwa huo ni ''nadra'' na kuwa faia ya chanjo ni kubwa zaidi kuliko athari maya za chanjo.

Taarifa rasmi kuhusu sababu ya kifo bado haijatolewa.

Hatahivyo, Bodi inayoshughulikia usalama wa chanjo ya Covid-19 imesema kuwa maumivu ya misuli ya moyo ''pengine yalitokana na chanjo''.

"Hii ni kesi ya kwanza huko New Zealand ambapo kifo kimehusishwa na chanjo ya Pfizer COVID-19. Wakati Kituo cha Ufuatiliaji wa athari mbaya kimepokea ripoti nyingine za vifo kwa mtu aliyepewa chanjo ya hivi karibuni, lakini hakuna taarifa ya kifo inayohushwa na chanjo, "kilisema katika taarifa.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad