google-site-verification: googleb0bc30c3e5fdb812.html Ole Sabaya Aanza Kujitetea Mahakamani | UDAKU SPECIAL

Ole Sabaya Aanza Kujitetea Mahakamani

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA





Mshtakiwa wa kwanza katika kesi ya unyang'anyi kwa kutumia silaha aliyekuwa Mkuu wa wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro Lengai Ole Sabaya ameanza kutoa utetezi wake  jana  katika mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha .


Akitoa utetezi wake mbele ya Hakimu mkazi Mwandamizi Odira Amworo akiongozwa na wakili  wake Moses Mauna mstakiwa huyo Lengai Ole Sabaya ameielezea mahakama kuwa  mnamo tarehe tisa mwezi wa pili 2021  alikuwa Bomang'ombe makao makuu ya wilaya ya Hai  na alikuwa  anaongoza kikao cha kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya  kuanzia asubuhi saa tatu na nusu hadi saa nane na nusu mchana.  

Sabaya amesema kuwa baada ya kumaliza kikao hicho saa nane mchana hadi saa tisa kasoro alipokea maelekezo na mamlaka za uteuzi ikamtaarifu kuwa kuna watu wameshuka Uwanja wa Ndege wa KIA na alipaswa  kuwachukua na kuambatana nao kwaa ajili ya kuwafikisha mkoani  Arusha.

Ndipo baada ya hapo aliwatafutia gari huku akiwa na gari lake binafsi ambalo alikuwa anaendeshwa na dereva wake huku jumla wakawa na magari mawili nakuanza safari kwenda Arusha huku aliokuwa amewachukua walikuwa na taarifa walichoagizwa huko Arusha.

Amesema mahakamani kuwa ilipofika saa saa kumi na moja na dakika arobaini na tano jioni walifika Arusha  baada ya kufika walienda eneo ambalo walielekezwa kwa ajili ya kufanya mahojiano na muhusika  ambae ni mmliki wa duka la shahidi Store Muhamed Saad  lakini hakumkuta.

amesema baada ya kumkosa mmiliki huyo licha ya watu hao waliongozana nao ambao hakuwataja mahakamani hapo na kudai hawahusiki na shitaka hilo walikuwa na taarifa zote kwamba watamkuta mmiliki huyo.

Sabaya amesema kuwa  baada ya kumkosa mmiliki huyo alifanya mawasiliano na mamlaka waliopewa maelekezo hayo kisha ikawaambia kuwa wameshafanya mawasiliano na Mkuu wa Wilaya ya Arusha hivyo hao watu waliowakuta katika duka hilo wapelekwe kituo cha polisi kwa sababa watasaidia kupatikana kwa muhusika na yeye akaelekezwa kuwasiliana nae huyo mkuu wa wilaya.

Akaeielezea mahakama kuwa mshtakiwa wa pili Silvesta Nyegu hakuwepo katika tukio hilo na mshtakiwa wa tatu Daniele Mbura hamfahamu kabisa na wala hajawahi kuonana nae maisha yake yote .

Amesema kuwa Bakari Msangi hakupigwa kama anavyodai na alichokielezea mahakamani hapo ni uongo na yeye hamfahamu kama amepigwa na kwamba Bakari Msangi ameamua kufanya hivyo kutokana na ugomvi wa kisiasa wa muda mrefu baina yake na yeye baada ya  kumshinda katika uchaguzi wa kiti uwenyekiti wa umoja wa wavijana chama cha mapinduzi yeye pamoja na wenzake.

Hakimu mkazi Mwandamizi Odira Amworo ameahirisha kesi mpaka Jumatatu tarehe 16 Agosti 2021 ambapo mshatakiwa huyo ataendelea kutoa utetezi wake.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad