Rais akimbia nchi baada ya wanamgambo wa Taliban kuufikia mji mkuu

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Rais Ashraf Ghani ameondoka nchini kwake, taarifa zinasema zimenukuu maofisa wa Afghan.
Taarifa ya kuondoka kwake imekuja mara baada ya Taliban ilivyofikia katika pembezoni mwa Kabul.

Makamu wa rais Amrullah Saleh naye aripotiwa kuondoka.

Taarifa za Bwana Ghani kuondoka zimekuja wakati ambao kumekuwa na mvutano mkubwa wa miji yote mikuu ya Afghanistan kudhibitiwa na wanamgambo wa Taliban.

Ofisi ya rais imeiambia Reuters kuwa "hawawezi kusema lolote kuhusu kuondoka kwa rais Ashraf Ghani kwasababu za kiusalama".

Wakati huohuo msemaji wa Taliban ameiambia BBC "hakutakuwa na visasi kwa watu wa Afghanistan.

Suhail Shaheen amewaakikishia wananchi kuwa ;"Tunawahakikishia raia wa Afghanistan, haswa wa mji wa Kabul, kuwa mali zao na maisha yao yatakuwa salama - hakuna atakayelipa kisasi kwa yeyote.

"sisi ni watumishi wa watu wa taifa hili."

Raia wengi wa Afghans wanahofia kurejea kwa ukatili uliofanyika mwaka 1990, ambapo watu waliuawa, walipigwa mawe na wasichana walipigwa marufuku kwenda shule.

Wanamgambo wa Taliban wamekaribia kuithibiti nchi nzima ya Afghanistan, huku mji mkuu wa nchi hiyo Kabul ukiwa umedhibitiwa pia na serikali.

Mapema leo Jumapili wanamgambo hao wameinyakua Jalalabad, bila mapigano. Jiji hilo lipo Mashariki mwa nchi.

Hatua hiyo ilifuatia kudhibitiwa kwa kwa mji muhimu wa shughuli za kiseriali wa Mazar-i-Sharif uliopo kaskazini hapo jana Jumamosi.

Kuzidiwa haraka kwa vikosi vya majeshi ya serikali kumemuweka Rais Ashraf Ghani katika shunikizo kubwa la kujiuzulu.

Rais Ghani anaonekana yupo njia panda katika kuamua la kufanya kati ya kujisalimisha au kuendeleza mapambano ya kudhibiti makao makuu ya nchi, Kabul.

Wakati huohuo, Marekani imeanza kuwaondoa wafanyakazi wake wa ubalozi jijini Kabul. Jumapili asubuhi wafanyakazi hao wamepelekwa uwanja wa ndege ambako wameonekana wakipanda ndege sita kubwa za kijeshi. Marekani imepeleka wanajeshi 5,000 kusaidia operesheni hiyo.

Rais Joe Biden ametetea uamuzi wa kuongeza kasi ya Marekani kuondoka Afghanistan, akisema hawezi kuhalalisha uwepo wa Marekani Afghanistan bila kikomo huku nchi hiyo ikikabiliwa na mgogoro mkubwa wa ndani.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad