Ronaldo: 'Nimerudi kwa ajili yako Sir Alex Ferguson'

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Cristiano Ronaldo ametambulishwa rasmi leo na kusema "amerudi nyumbani" kwenye klabu yake ya Manchester United na akisema amerejea nyumbani kwa bosi wake wa zamani Sir Alex Ferguson.
United imelipa dau la £12.85m kumsajili mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 36 kutoka Juventus, muongo mmoja baada ya kuondoka klabu hiyo kujiunga na Real Madrid.

Amesaini mkataba wa miaka miwili, huku akiwa na nafasi ya kuongeza mwaka mwingine mmoja.

"kila mtu ananijua, wanajua mapenzi yangu yasiyokwisha kwa Manchester United," aliandika kwenye mtandao wake wa Instagram.

"Ni kama ndoto vile, baada ya mara kadhaa kucheza dhidi ya Manchester United, tena kama mpinzani, lakini bado naona mapenzi na heshima kutoka kwa mashabiki jukwaani.

Mshindi huyo mara tano wa tuzo ya mchezaji bora wa dunia ‘Ballon d'or anasema: "Nipo apa, imrejea nyumbani! Tupambane kwa mara nyingne! - Sir Alex, hii ni kwa ajili yako…"

Sir Alex Ferguson alikuwa meneja wa United wakati Ronaldo anacheza Old Trafford, na kufunga mabao 118 katika mechi 292 kabla ya kutimkia Real Madrid mwaka 2009.

Inaaaminika alizungumza na Ferguson kabala ya kuamua kutua United.

Meneja mpya wa mashetani hao wekundu Ole Gunnar Solskjaer alisema: "Unakosa maneno unapomuelezea Cristiano. Sio mchezaji mzuri na wa ajabu, lakini pia ni mtu mzuri.

Ronaldo anaweza kuwepo kwenye mchezo wa United dhidi ya Newcastle United Septemba 11, utakua mchezo wa kwanza kuchezwa na klabu hiyo baada ya mapumziko ya mechi za kimataifa.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad