Mbowe na wenzake wasomewa mashtaka upya

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe na wenzake watatu wasomewa upya mashtaka yao sita mbele ya Jaji Mustapha Siyani 
Mbowe na wenzake wamefikishwa katika Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi leo Ijumaa Septemba 10, 2021 ambapo kwa mara ya kwanza Leo wataruhusiwa na Mahakama hiyo kujibu tuhuma zinazowakabili kwa kusema ndio wanakubaliana na tuhuma au hapana hawakubaliana na tuhuma hizo.

Mbowe anashtakiwa pamoja na Halfan Bwire Hassan, Adamu Hassan Kasekwa maarufu kama Adamoo na Mohamed Abdillahi Ling’wenya ambao wote ni makomandoo waliofukuzwa kazi jeshini kutokana na sababu mbalimbali. Watuhumiwa wanakabiliwa na mashtaka sita, likiwamo la kukutwa na sare na vifaa vya Jeshi la Wananchi (JWTZ). Wanadaiwa kutenda makosa hayo kati ya Agosti mosi na Agosti 5 mwaka jana.

Vilevile wanatuhumiwa kupanga vitendo vya kigaidi ambavyo ni kulipua vituo vya mafuta na maeneo ya mikusanyiko na kumdhuru aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad