Ulaya yasema Iran iko tayari kurejea kwenye mazungumzo ya nyuklia

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA





Mkuu wa sera za kigeni wa Umoja wa Ulaya, Josep Borell amesema mwanadiplomasia wa ngazi ya juu wa Iran amemuhakikishia kwamba nchi hiyo iko tayari kuanza tena mazungumzo kuhusu makubaliano ya nyuklia hivi karibuni. 
Taarifa ya Umoja wa Ulaya imesema leo kuwa Borrell alisisitiza kwa mara nyingine tena umuhimu mkubwa wa kuanza mazungumzo ya Vienna katika mkutano uliofanyika jana kati yake na Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Hossein Amir-Abdollahin pembezoni mwa mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa. 

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Amir-Abdollahin amehakikisha utayari wa kuanza tena mapema kwa mazungumzo. 

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Saeed Khatibzadeh amesema anatarajia mazungumzo hayo yataanza tena katika wiki zijazo, bila ya kutaja tarehe kamili.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad