Wafungwa zaidi ya 200 wametoroka gerezani Nigeria, Baada ya watu wenye silaha kuvamia

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Maafisa katika jimbo la Nigeria la Kogi 240 wametoroka baada ya watu wenye silaha kuvamia gereza katika eneo la Kabba-Bunu. Mamlaka ya huduma za magereza nchini Nigeria inasema kuwa washambuliaji walikuwa wamejihami kwa silaha.


 
Kuna taarifa ambazo hazijathibitishwa kuwa maafisa wawili wa usalama waliuawa wakati wa tukio hilo.

Taarifa zinasema wakati wavamizi walipofika, walikabiliana na walinzi wa gereza, na ndipo walipofanikiwa kuingia ndani ya gereza baada ya kuwazidi nguvu maafisa wa usalama wa ngereza hilo.

Maafisa bado hawajatoa taarifa kuhusu idadi ya watu waliouawa au majeruhi katika makabiliano hayo yaliyotokea Jumapili usiku.

Mamlaka ya huduma za magereza nchini Nigeria imesema kuwa kulikuwa na jumla ya wafungwa 294 katika gereza hilo wakati shambulio lilipotokea, 240 kati yao walikuwa wakisubiri kesi zao, na 70 walikuwa tayari wamehukumiwa.

Kamishna mkuu wa magereza Halliru Nababa tayari amekwishaagiza kukamwatwa wafungwa waliotoroka.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad