Wahamiaji 20 kutoka Morocco wafariki-baharini

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Wahamiaji 20 wasio wa kawaida waliojaribu kufika kwenye Visiwa vya Canary kusini-magharibi mwa Uhispania kutoka pwani ya Morocco walipoteza maisha baharini.
Kulingana na shirika la habari la Uhispania EFE, likinukuu vyanzo vya Utawala wa Uhuru wa Visiwa vya Canary, mashua iliyobeba wahamiaji wasio wa kawaida, ambayo iliondoka pwani ya mji wa Tan-Tan wa Morocco mnamo Agosti 27, ilifikia Bandari ya Rosario kwenye Kisiwa cha Fuerteventura.

Mamlaka ilitoa taarifa kuwa wahamiaji 15 wa kiume na 16 wa kike walitoka kwenye mashua.

Kulingana na taarifa za wahamiaji, wahamiaji 20 kwenye mashua walipoteza maisha wakati wa safari na miili yao ilitupwa baharini.

Ilibainika kuwa wahamiaji wasio wa kawaida wenye asili ya Kiafrika ambao walifika Uhispania walipelekwa kwenye makao hayo.

Hivi karibuni, kumekuwa na ongezeko kubwa la uhamiaji usio wa kawaida kutoka pwani za Afrika Kaskazini hadi Visiwa vya Canary.

Zaidi ya wahamiaji 8,300 kwenye boti au mashua 230 walikwenda Visiwa vya Canary mwaka huu, na kuongezeka  kwai asilimia 150 ikilinganishwa na mwaka jana.

Zaidi ya wahamiaji 230 wamekufa kwa kuzama majini mwaka huu wakielekea Visiwa vya Canary, kulingana na data rasmi.

Wawakilishi wa mashirika yasiyokuwa ya kiserikali wanasema kuwa idadi ya waliokufa inaweza kuwa kubwa zaidi kwani kuna boti nyingi ambazo ziliondoka kutoka pwani za Afrika Kaskazini lakini hazijulikani

OPEN IN BROWSER
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad