Jamaa Anaswa Akichepuka na Mke wa Mtu, Afungwa Kwenye Gunia

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA





Kisanga cha aina yake kimezuka katika eneo moja mjini Embu nchini Kenya baada ya jamaa kufungwa kamba miguuni na kutiwa ndani ya gunia hadi alipe faini baada ya kufumaniwa akichepuka na mke wa rafiki yake.

 

Taarifa kutoka nchini humo zimearifu kwamba jamaa huyo alikuwa na tabia ya kumyemelea mke wa rafiki yake wakati mume huyo akiwa zamu ya usiku kazini.

 

Njemba huyo alifika kwa rafiki yake na kumkuta mkewe akiandaa chakula cha jioni. Kwa kuwa mrembo huyo hakuwa na watoto pale nyumbani, jamaa alichukua fursa hiyo kumrushia mistari ya mapenzi.

 

Wawili hao walikubaliana na kuzama katika boma la nyumba ambalo halijaisha pale pale nyumbani ili kutenda amri ya sita, lakini wakiendelea na mambo yao, ghafla mtu aliingia kwenye boma hilo.

 

Alikuwa ni mke wa dada yule, jamaa alipoingia ndani hakuamini macho yake, moyo wake ulimdunda kwa mshtuko akatokwa na jasho shingoni. Naye mwizi wa mke wa jamaa akaduwaa na huku akibaki mdomo wazi kwa kufumaniwa.

 

“Ala! Ni wewe unamnyemelea mke wangu! Usishtuke, tulia tu. Sina haraka,” mume wa mtu alisema huku akiufunga mlango. Jamaa kwa upande wake alianza kuomba msamaha ila dua zake ziliambulia patupu.

 

Mwenye nyumba alichukua gunia kubwa na kamba, alimfunga jamaa yule miguuni na kumtia kwenye gunia bila jamaa kulalamika. Mke wa jamaa naye alijikunyata kama kuku aliyenyeshewa huku akitetemeka kwa woga. Lofa alipigwa viboko kadhaa kama ngoma huku akipigiwa mayoni kwa kile alichokifanya.

 

“Kama unataka amani utafanya mambo mawili sasa hivi ili nikiachilie. Kwanza utalipa faini ya KSh 100,000 kwa kumnyemelea mke wangu. Pili utamchukua mke wangu awe mke wako na unirudishiea mahari niliyomlipia,” jamaa alisema.

 

“Nimegindua wewe sio mwanamke mwaminifu. Chukua kilicho chako na uende kabisa. Sikutaki tena,” jamaa alimwambia mkewe. Taarifa zinadai kwamba jamaa alipopatiwa masharti makali na mwenzake, aliomba nafasi ya kuwapigia jamaa wamchangie pesa ili alipe faini ya maradi aachiliwe huru.

 

Wakati jamaa alipokuwa akiwashawishi wenzake wamchangie mke wa jamaa alikuwa chumbani akikusanya virago vyake ajipange kuondoka.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. HELLO GET OUT OF FINANCIAL MESS WITH THE HELP OF drbenjaminfinance@gmail.com

    I have been in financial mess for the past months, I’m a single mum with kids to look after. My name is REBECCA MICHAELSON, and am from Ridley Park, Pennsylvania. A couple of weeks ago My friend visited me and along our discussion she told me about DR BENJAMIN OWEN FINANCE of drbenjaminfinance@gmail.com that he can help me out of my financial situation, I never believed cause I have spend so much money on different loan lenders who did nothing other than running away with my money. She advised, I gave it a try because she and some of her colleagues were rescued too by this Godsent lender with loans to revive their dying businesses and paying off bills. so I mailed him and explain all about my financial situation and therefore took me through the loan process which was very brief and easy. After that my loan application worth $278,000.00USD was granted, all i did was to follow the processing and be cooperative and today I am a proud business owner sharing the testimony of God-sent Lender. You can as well reach him through the Company Email drbenjaminfinance@gmail.com

    THANK YOU VERY MUCH

    ReplyDelete

Top Post Ad