Kutunza Pesa na Kuzitupa Chini ni Kosa la Jinai

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Wizara ya Katiba na Sheria imewatahadharisha baadhi ya watu ambao wanatupata fedha chini wakati wa kutoa zawadi kwenye sehemu zozote za tafrija, kwani kwa kufanya hivyo ni kosa kisheria na atakayekamatwa kwa kufanya kosa hilo atashtakiwa kwa kufanya kosa la jinai.

Hayo yamebainishwa na Waziri wa Katiba na Sheria Profesa Palamagamba Kabudi, wakati akiongea na wazazi, wanafunzi pamoja na walimu wa shule ya sekondari ya Kilimo Kilosa mkoani Morogoro ambayo ni elimu jumuishi.

“Nadhani wengi hamfahamu, kutupa, kuikunja au kuichana fedha ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni kosa la jinai, acheni kutupa fedha, fedha sio karatasi tena ina alama ya Baba wa Taifa, maana yake unamtupa Baba wa Taifa chini?” amesema Prof. Palamagamba Kabudi, Waziri wa Katiba na Sheria.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad