Maskini Akothee Arudishwa TENA Hospitalini ni Baada ya Siku Chache Kuruhusiwa Kurudi Nyumbani, Afunguka Haya

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Mwanamuziki mashuhuri wa Kenya Esther Akoth ambaye hujulikana kama Akothee amefichua kwamba alikaa siku ya Jamhuri alikuwa hospotali baada ya kulazwa tena.

Kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram akithibitisha kisa hicho, alipakia picha kadhaa akidai kwamba hakuwa na wakati wa kutumia siku yake ya Jamhuri na familia yake.

Hii Inasemekana ilitokea siku chache baada ya kudaiwa kuruhusiwa kutoka katika hospitali alikokuwa amelazwa kwa muda.

Siku chache zilizopita, Akothee alifichua kuwa alilazwa baada ya kuugua ugonjwa unaojulikana kama ND ambao ni uharibifu wa neva unaosababisha mishipa ya fahamu ya mtu kuhisi ganzi na baada ya hapo inadaiwa kuvimba.

Baada ya kupakia Picha akiwa kwenye kitanda cha hospitali aliandika ujumbe huu;

✍“Siwezi kuelezea kile kinachonila, lakini kinaendelea kufanya jambo lake kwa wakati mbaya zaidi. Tumekuwa hapa tangu Jumamosi na hii ni sherehe yetu ya jamhuri. Leo naweza kuinua kichwa changu 💪” Akothee Aliandika

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad