Shahidi Akwamisha KESI ya Mbowe

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




KESI ya uhujumi uchumi, inayomkabili Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na wenzake, imeahirishwa hadi Jumatano, tarehe 26 Januari 2022, kutokana na shahidi wa Jamhuri kupata udhuru. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar ea Salaam … (endelea).

Kesi hiyo inayosikilizwa mfululizo imeahirishwa na Jaji Joachim Tiganga, baada ya Kiongozi wa Jopo la Mawakili wa Mashtaka, Wakili wa Serikali Mwandamizi, Robert Kidando, kuomba ahirisho akidai shahidi waliyekuwa wanamtegemea amepata dharura na kushindwa kutoka mkoani kuja Dar es Salaam, ilipo mahakama hiyo.

Mbali na Mbowe, washtakiwa wengine katika kesi hiyo yenye mashtaka ya ugaidi, ni waliokuwa makomandoo wa Jeshi la wananchi wa Tanzania (JWTZ), Halfan Bwire Hassan, Adam Kasekwa na Mohammed Abdillah Ling’wenya.

Jaji Tiganga aliuamuru upande wa mashtaka umlete shahidi siku hiyo, ili kesi hiyo iendelee kusikilizwa.



-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad