AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe amesema amemuomba Mkuu wa Wilaya ya Kibaha amtafute Mkazi wa Kongowe Wilayani Kibaha Halfani Issa (42) na kumsadia kupitia SIDO, baada ya kuripotiwa kwa taarifa za Halfani kukamatwa na Polisi Mkoani Pwani kwa kosa la kumiliki na kuendesha kiwanda bubu cha kuchakata mafuta ya maweze bila kuwa na kibali.
"Nimewasiliama na Mh DC wa kibaha nimemuomba amtafute huyu Mwananchi (Halfani na kumsaidia kupitia SIDO na Wizara ya Kilimo tuna promote “Value addition” through backyard processing hana tofauti na wale wa alizeti wanaouza Barabarani ni Jukumu letu kuwasaidia"
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani Wankyo Nyigesa wakati wa zoezi la kukamatwa kwa Halfani alisema wamemkamata yeye pamoja na madumu zaidi ya tisini yaliyojazwa mafuta ya mawese na akasema watashirikiana na Mamlaka nyingine za Serikali kama TMDA,TBS na OSHA ili kuweza kujua athari zinazoweza kupatikana.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK