Huu ndio mwisho wa Russia ya sasa ya Putin - Akunin

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Mwandishi wa masuala ya uhalifu wa Kirusi mwenye vitabu vilivyouzwa zaidi Boris Akunin ametabiri uvamizi wa Ukraine ndio mwisho wa Putin na kwamba Warusi lazima wajumuike pamoja ili kuwasilisha Urusi nyingine, bora zaidi kwa ulimwengu na kufanya kila wawezalo kuwasaidia wakimbizi wa Ukraine.

Pamoja na gwiji wa densi Mikhail Baryshnikov na mwanauchumi Sergei Guriev, ameanzisha mpango wa kukusanya pesa kwa ajili ya wakimbizi wa Ukraine unaoitwa TrueRussia.org.

Boris Akunin, ambaye jina lake halisi ni Grigory Ckhartishvili, ndiye mtunzi wa riwaya maarufu za upelelezi za Fandorin na ameishi Uingereza tangu 2014. Mikhail Baryshnikov alihama kutoka Umoja wa Kisovieti na kwenda Canada mwaka wa 1974 na Sergei Guriev ni profesa wa uchumi wa Paris ambaye alikimbia Urusi mwaka wa 2013.

Akunin aliambia BBC kwamba vituo vya TV vya Ukraine vilikuwa vikimpigia simu kila siku ili aonekane kwenye vipindi vyao.


 
"Lakini sasa lazima nizungumze na Warusi. Labda hatuwezi kusimamisha vita, lakini tunaweza kusaidia katika mzozo wa kibinadamu, na lazima tuungane na kufanya kila tuwezalo kumuondoa Putin, ili tuweze kuijenga tena Urusi ya kawaida. ”

Akunin alisema Warusi wote waliofanya vyema baada ya kuanguka kwa Umoja wa Kisovieti walishiriki jukumu la utawala wa sasa na wanapaswa sasa kukabiliana na ukweli mpya.

"Ninahisi ninaishi katika riwaya ya kikale na kwa mara ya kwanza tangu kuanguka kwa Muungano wa Sovieti, ninaogopa kuna tishio la kweli la vita vya nyuklia."

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad