Mama Kanumba "Nisaidieni Udhamini Nifanye Movie ya Kanumba"

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



MAMA wa aliyekuwa staa mkubwa wa filamu za Kibongo, marehemu Steven Kanumba, Flora Mtegoa anasema kuwa, hakuna kitu ambacho anakitamani kama kutengeneza makala maalum ya Kanumba tangu utotoni hadi kifo chake.


Anasema kuwa, akifanikiwa ataona kuwa kuna kitu kikubwa amekifanya kwa mtoto wake, lakini ukweli ni kwamba hajui ataanzia wapi kwa sababu hana pesa hivyo anaomba udhamini kwa ajili ya kazi hiyo.


Akizungumza na Gazeti la IJUMAA, Mama Kanumba anawaomba wadhamini mbalimbali ambao wanaweza kumuwezesha kwa namna moja au nyingine kuweza kufanya makala hiyo ya mtoto wake kwa sababu itabaki kuwa ni kumbukumbu nzuri kwa vizazi vijavyo.


“Kuna kitu kikubwa ninakitamani sana na hakika roho yangu itatulia sana kama nitaweza kufanya makala ya mwanangu hivyo nawaomba wadau mbalimbali kama wapo waje wanisaidie au tushirikiane kwa jambo hilo, hakika nitakuwa nimeiponya nafsi yangu kwa mawazo,” anasema mama huyo ambapo bado mwezi mmoja Kanumba atumize miaka kumi tangu atangulie mbele ya haki.


Kanumba alifariki dunia siku ile ya Aprili 7, 2012 akiwa ndiye kinara wa Bongo Movies.

Stori; Imelda Mtema, Dar
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad