Muna Love "Mungu Amenitoa Kwenye Umauti"

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



ROSE Alphonce Nungu almaarufu Muna Love; ni mwigizaji wa Bongo Movies ambaye hajaonekana lokesheni kitambo ambaye anasema kuwa, kila siku anamshukuru Mwenyezi Mungu kwa sababu amemuinua na kumtoa kwenye umauti kisha kumrejesha uzimani.

Muna anasema kuwa, jambo hilo hakulitegemea kabisa katika maisha yake kama atasimama tena.

Hii ni baada ya kufanyiwa upasuaji (sajari) sehemu mbalimbali za mwili wake kwa ajili ya kurekebisha maumbile yake.

Akizungumza na Gazeti la IJUMAA kwa njia ya WhatsApp akiwa nchi za nje, Muna anasema kuwa, alipita katika mapito magumu mno kiasi cha kukata tamaa, lakini Mungu amemsaidia na ameinuka na hivi karibuni atarejea tena.


“Mungu amenitoa kwenye umauti, nitarejea tena nikiwa na hofu ya Mungu. Niliyopitia ni funzo kubwa sana katika maisha yangu na nikitulia nitaelezea yote bila woga na hapo mtu ataamua kujifunza mwenyewe,” anasema Muna ambaye hivi sasa anaonekana kupona kabisa.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad