Ukraine yadai kudungua ndege tatu za kivita za Urusi na kuyaangusha makombora mawili

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Jeshi la Ukraine limetoa taarufa kwa vyombo vya Habari likisema kwamba limefanikiwa kufanyia uharibifu mkubwa makundi ya jeshi ya Urusi.


Linasema kwamba jeshi lao la angani lilifanikiwa kudungua ndege tatu za kivita za Urusi , helikopta moja , ndege tatu zisizo na rubanina kuyaangusha makombora mawili. BBC bado haijaweza kuthibitisha madai hayo.


Jeshi la Ukraine pia limesema kwamba huku Urusi ikiendelea kushambulia maeneo yalio na wakaazi wengi mijini, wanajeshi wake wameshindwa kusonga mbele , ikiwemo katika maeneo ya Donetsk, Luhansk na Mykolaiv.


‘’Adui anaendelea kupata hasara katika maeneo fulani’’, taarifa hiyo ilisema.


Chapisho la mapema , lilisema kwamba jeshi la Urusi limeshindwa kuyadhibiti maeneo iliyoyateka na kwamba lilikuwa linakaribia kuwaita makadeti wake kwenda katika mstari wa mbele katika vita.


Urusi pia inatafuta wapiganaji wa kigeni ili kufidia maeneo ambayo wanajeshi wake wameuawa ama hata kusalimu amri.


Waziri wa Ulinzi nchini Uingereza katika taarifa yake alisema kwamba : Kutokana na hilo hasara waliopata imeifanya Urusi kushindwa kutekeleza mashambulizi wakati ambapo wanajeshi wa Ukraine wamejizatiti kujibu mashambulizi.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad