google-site-verification: googleb0bc30c3e5fdb812.html Pablo Anena Ushindi Dhidi ya Orlando Kisha Aguna "Tumejiweka Pazuri ila Kwao mmh" | UDAKU SPECIAL

Pablo Anena Ushindi Dhidi ya Orlando Kisha Aguna "Tumejiweka Pazuri ila Kwao mmh"

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Kocha Mkuu Pablo Franco, ameweka wazi furaha yake ya ushindi wa bao moja nyumbani waliopata dhidi Orlando Pirates akisema unampa faida kwenye mchezo wa marudiano wiki ijayo nchini Afrika Kusini.


Pablo amesema michuano ya Afrika ni migumu hivyo unapaswa kutumia vema uwanja wa nyumbani ili kujiweka katika mazingira mazuri kwenye mchezo wa marudiano.


Pablo ameongeza kuwa wanatarajia kupata upinzani mkubwa kutoka kwa Orlando kwenye mchezo wa marudiano lakini wamejipanga kuhakikisha wanaenda kufanya vizuri ugenini.


Pablo amekiri kuwa hawakuwa na matokeo mazuri kwenye mechi za ugenini katika hatua ya makundi kwa hiyo wanapaswa kujipanga hasa kutokana na ubora wa wapinzani.


“Michuano ya Afrika mara nyingi timu zinafanya vizuri nyumbani kama tulivyofanya. Tutajipanga kuelekea mchezo wa marudiano ugenini tunahitaji kufuzu nusu fainali,” amesema Pablo.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad